Wigo
Kibaha Folk Development College
Chuo
cha Maendeleo ya Wananchi Kibaha (KFDC) kilianzishwa mwaka 1964 kama
Chuo cha Wakulima (Farmers Training Centre) kikiwa ni chombo
kimojawapo cha kutekeleza moja ya madhumuni makuu matatu ya
kuanzishwa kwa Shirika la Elimu kibaha ambalo ni kukabiliana na adui
umaskini kwa wananchi toka mikoa ya Tanga, Morogoro, Pwani na Dar es
Salaam. Mwaka 1975, Chuo kilibadilishwa jina na kuitwa Chuo cha
Maendeleoo ya Wananchi Kibaha. Malengo na shabaha zake ziliendelea
kubaki zile zile za kutokomeza umaskini pamoja na kuwa Chuo Mama cha
Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi Tanzania. Kama Chuo Mama, KFDC,
kiliongezewa majukumu ya kufundisha wakufunzi wapya wanaojiunga na
vyuo vya Maendeleo ya Wananchi (VMW) falsafa na njia za kumfundisha
mtu mzima. Kuendesha Warsha na semina kwa walimu na watumishi wa
VMW. Warsha na semina zilihusu uboreshaji wa taaluma na utendaji
bora wa kazi katika VMW. Mwaka 1992 Chuo kiliacha kuwa na kujumu la
kuwa Chuo Mama.
Mafunzo Yanayotolewa na Chuo
Chuo kina uwezo wa kupokea jumla ya wanachuo 200 kwa mwaka. Bweni 128 na kutwa 72. Masomo yanayotolewa katika chuo cha KFDC ni kama yafuatayo:-
Fani ya Kilimo na Mifugo
Fani ya umeme wa majumbani
Fani ya uungaji na uundaji vyuma
Fani ya magari na mitambo
Fani ya ujenzi (useremala, uashi na bomba)
Fani ya ushonaji
Fani ya upishi
Wanachuo pia wanatakiwa kusoma masomo yanayohusiana na fani hizo ambayo ni:-
English and communication skills
Life skills
Entrepreneurship
Technical drawing
Mathematics
Computer science
Engineering science
French
Tourism
Quantitative methods.
Chuo pia hutoa kozi fupi ya udereva kwa muda wa miezi miwili na wahitimu hupata vyeti na kupelekwa kwa maafisa usalama barabarani kujaribiwa na hatimaye kupewa leseni.
Chuo hutoa mafunzo maalum (stadi) zinazopendekezwa na Halmashauri za Wilaya kwa wananchi wake. Mafunzo ya namna hiyo hugharimiwa na Halmashauri hizo.
Pamoja na mafuzo hayo Chuo hutoa huduma kwa ukodishaji wa kumbi kwa ajili ya Semina, sherehe nk na utoaji wa chakula na malazi kwa wanasemina hao.
Taratibu za Kujiunga na Chuo
Taratibu za kujiunga na chuo ni kwamba kwanza yanatolewa matangazo kwa kubandikwa kwenye mbao za matangazo kwenye ofisi mbalimbali, katika wilaya ya kibaha na pia kwenye makanisa na misikitini. Anayetaka kujiunga huchukua fomu na baadae kufanya usaili.