Wigo

Shule Ya Sekondari Tumbi

Shule ya Sekondari Tumbi ni kati ya Taasisi za Shirika la Elimu kibaha.  Ipo kilometa 4 kutoka kwenye kitovu cha mji wa halmashauri ya mji Kibaha (Maili Moja) au kilometa moja kutoka katika kijiji cha Picha ya Ndege.

Shule ilianza rasmi mwaka 1999 ikiwa na idadi ya wanafunzi 30 tu, wasichana 13  na wavulana 17 ikiwa na mkondo mmoja (1) na mpaka leo hii shule ina idadi ya wanafunzi 578, ikiwa na wasichana 231 na wavulana 347.  Kwa sasa shule ina jumla ya mikondo 16, kwa kila kidato.

Shule ina jumla ya wafanyakazi 43 miongoni mwao walimu wakiwa 37 na watumishi wasio walimu 06.  Kati ya walimu hao wenye shahada za uzamili ni 05, shahada 18 na stashahada ni 12.

Shule ya sekondari Tumbi ni ya mchepuo wa sayansi, biashara na maarifa ya nyumbani, hivyo masomo yanayofundishwa katika shule hii ni:

1. CIVICS  2. ENGILSH  LANGUAGE  3. KISWAHILI  4. GEOGRAPHY  5. HISTORY  6. BIOLOGY  7. BASIC MATHEMATIC  8. PHYSICS  9. CHEMISTRY   10. COMMERCE     11   BOOK KEEPING  12. FOOD AND NUTRITION

MAFANIKIO YA SHULE KITAALUMA

Taaluma ya shule ya Sekondari Tumbi imezidi kupanda mwaka hadi mwaka kama ifuatavyo:-

                                              

MWAKA

% YA UFAULU

2009

82

2010

84

2011

79

2012

37