Habari

WANAFUNZI WA SHULE YA SEKONDARI KIBAHA WACHANGIA DAMU KWA AJILI YA HOSPITALI YA TUMBI


WANAFUNZI WA SHULE YA SEKONDARI KIBAHA WACHANGIA DAMU KWA AJILI YA HOSPITALI YA TUMBI

Na: Lucy Semindu Kibaha

Tarehe 19 Januari, 2017

Kitengo cha damu Salama cha Hospitali ya Tumbi leo wapo katika  Shule  ya Sekondari Kibaha ambapo wanafunzi wa Shule hiyo wanajitolea damu kwa ajili ya kuokoa maisha ya wananchi wenye uhitaji mkubwa wa damu .

Kila mwaka wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Kibaha wamekuwa na desturi ya kuchangia damu kwa ajili ya wagonjwa wanaokuja katika hospitali ya Tumbi .Shukrani zimwendee Mkuu wa Shule hiyo Bw. Chrisdom Ambilikile kwa kuhamasisha vijana hao kujitolea kwa maslahi ya Taifa.